Posts

Tazama ajali ilivyokwamisha ndoto za kijana huyu

Image
Na Adrian Mgaya. Inasikitisha kwa kweli Ketson John, aligongwa na pikipiki ikamkata mguu na kumtupia kwenye mataluma ya reli, kabla hata hajainuka treni ikampitia na kumkata mguu uliosalia... Mtazame hapa kupata undani wa maisha yake.

KWANINI SHERIA HAIWABANI WANAOKAA VITI VYA NYUMA KUFUNGA MKANDA?

Na Adrian mgaya Shirika la afya duniani linataja viashiria vikuu vya ajali za barabarani kuwa ni kutokuvaa kofia ngumu kwa waendesha pikipiki, mwendokasi usiofaa, matumizi ya vilevi kwa madereva, kutotumia vizuizi vya watoto na kutofunga mkanda wa usalama katika vyombo vya usafiri. Pamoja na viashiria hivi kutajwa kuwa ni vyanzo vikuu vya ajali na kuongezeka kwa madhara ya ajali za barabarani bado sheria mama ya usalama barabarani nchini Tanzania, haijagusia kiundani mambo haya ili kuendana na matakwa ya umoja wa mataifa kupitia shirika la afya duniani. Ambapo wanapendekeza sheria madhubuti zitasaidia kupunguza vifo na majeruhi wa ajali katika barabara zetu. Edda sanga, Mkurugenzi mtendaji wa TAMWA anasema "Umoja wa mataifa na shirika la afya duniani wanakiri kwamba sheria madhubuti zinahitajika katika kupunguza idadi ya watu wanaofariki katika barabara zetu. Tanzania lazima tuwe na sheria kali za usalama barabarani kukomesha hali hii” Sheria ya usalama barabarani ya m...

JE, UNAFAHAMU HATARI YA KUENDESHA GARI USIKU?

Image
Na Adrian Mgaya Licha ya kwamba uono wa usiku ni hafifu kuliko mchana baadhi ya madereva hukimbilia kuendesha usiku, tena katika mwendo ambao ni hatari kwa maisha yao abiria na watembea kwa miguu...  Makala hii ni matokeo ya mradi wa mafunzo ya uandishi wa habari za usalama barabarani (Bloomberg initiative for Global road safety-BIGRS : Road safety journalism fellowship) yaliyofadhiliwa na shirika la afya duniani (WHO) na kutekelezwa na Tanzania Media foundation (TMF). Bofya video hii kutazama.

MATUKIO KATIKA PICHA: WIKI YA USALAMA BARABARANI.

Image
Na Adrian Mgaya Maandamano ya wadau wa usalama barabarani, wakiwa wamebeba mabango yenye ujumbe mbalimbali juu ya usalama barabarani. Katika ufunguzi wa wiki ya usalama barabarani katika viwanja vya mashujaa mkoani Kilimanjaro. Vijana wa haraiki wakitoa burudani wakati wa maadhimisho ya wiki ya usalama barabarani. Zahara Tunda (road safety fellow) akiwa katika majukumu ya ukusanyaji taarifa wakati wa maadhimisho ya wiki ya usalama barabarani.

"WANASIASA WA NAWAPA KIBURI WAENDESHA BODABODA MBEYA"

Image
Na Adrian Mgaya Baadhi ya madereva wa pikipiki na bajaj mkoani Mbeya ambao wengi wao wana umri chini ya miaka 35, wapo katika hatari ya kupata madhara yatokanayo na athari za ajali za barabarani kutokana na kuwa wakaidi kwa mamlaka zinazosimamia usalama barabarani. Butusyo Akimu Mwombelo ambaye ni mkuu wa kikosio cha usalama barabarani mkoa wa Mbeya anasema, ongezeko kubwa la ajali za barabarani linachochewa na madereva wa pikipiki na bajaj. Hata hivyo juhudi za kupambana na hali hiyo zina vikwazo vingi kutokana na mwingiliano na mambo ya siasa. Tazama video hii kufahamu zaidi.